Header Ads Widget

Kukaya Miono Yazindua Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024

Uzinduzi wa Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024Utangulizi

Umoja wa wana Kukaya Miono wilaya ya chalinze mkoani pwani, baada ya kuhitimisha mjadala wa elimu waliingia katika utekelezaji na hatua iliofuata ilikuwa ni kuchimba msingi wa chumba cha darasa shule ya msingi miono, zoezi ambalo liliisha vizuri na baada ya hapo wakapanga siku maalum kwaajili ya kuzindua ujenzi wa darasa hili.

Zoezi hili la uzinduzi lilihudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali na lengo likiwa ni kuweka jiwe la msingi, kutangaza malengo ya group la kukuya Miono na pia kutangaza harambee ya kuchangisha michango kwa wote watakaoguswa kwa namna moja ama nyingine kuungana na jitihada za wana kukaya Miono.

Hafla hio ilipangwa na viongozi wa group hilo akiwemo kiongozi mkuu na mwanzilishi wa group hili bwana Omari Mtiga na viongozi wengine wa group kama vile ndugu Sadiki Mchama, Juma Salum na wajumbe wengine.

Mgeni Rasmi.

Uzinduzi wa Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024

Mgeni rasmi wa shughuli alikuwa Mkurugenzi wa taasisi ya TETE Foundation Bi. Susan Senso ndie aliyeweka Jiwe la msingi akitangulizana na viongozi mbalimbali

Wageni waalikwaUzinduzi wa Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024

Mbali na mgeni rasmi wengine waliokuja kuwaunga mkono wana kukaya Miono ni umoja wa Kibindu Tunayoitaka ambao waliahidi kuchangia tofali 100 na kusema pia zinaweza zikazidi. Wengine pia walikuwa kutoka katika Kijiji cha Mkange ambao nao walihudhuria uzinduzi huu.

Tazama video ya wana kibindu wakiahidi kuchangia

Kwa ujumla kila kitu kilienda vizuri hapa chini ni baadhi ya picha kutoka eneo la tukio shule msingi Miono ambako uzinduzi ulifanyika.

Uzinduzi wa Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024
Uzinduzi wa Ujenzi wa Darasa shule ya msingi Miono Tarehe 10 Feb 2024


Post a Comment

0 Comments