
Waandishi maarufu wa habari za michezo Tanzania, Tullo Chambo (kushoto) na Ramadhani Mkandemba (kulia) wa gazeti la Tanzania Daima wakiwa na Mwanasoka Bora Anayecheza Afrika, Mbwana Ally Samatta (katikati) baada ya kuwasili Alfajiri ya leo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam kufatia kushinda tuzo hiyo ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) usiku wa juzi mjini Abuja, Nigeria

Wapenzi na mashabiki maarufu wa soka nchini, Esther na Bob Chicharito (kulia) walijitokeza pia kumlaki Samatta. Mshambuliaji huyo wa TP Mazembe ya DRC alipata mapokezi mazuri licha ya kuwasili usiku wa manane



Mwandishi maarufu wa habari za michezo, Mwani Nyangassa naye alijitokeza akiwa na fulana maalum ya "Hongera Samatta'
0 Comments