Header Ads Widget

Zitto Kabwe Amjibu Kubenea....Asema ni Mgonjwa wa Chuki, Muongo na Kigeugeu



==>Makala hii inapatika kwenye ukurasa wa Facebook wa Zitto Kabwe

MTUMISHI wa Mungu afumaniwe kwa uzinzi na mke wa mtu, kesho asubuhi aamkie madhabahuni kuhubiri neno kisha waumini wapokee. Huko ni kumtania Mungu.


Mimbari ni kwa ajili ya wasafi. Ukiwa mchafu hufai kuhubiri neno. Maneno ya Mungu hayashereheshwi na mwenye uchafu. Maana mtu mchafu ni mtenda dhambi.


Mwandishi wa Habari na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea, anataka kuhubiri neno. Waumini tunakataa. Maana asiye msafi hafai kuaminika kwa maneno yake.


Mhubiri neno hatakiwi kuwa ndumilakuwili. Hapaswi kuwa kigeugeu wala mshadadia uongo. Anatakiwa awe mkweli na siku zote aweze kuuishi ukweli wake.


Kubenea hana aibu kama Sepp Blatter, yule aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa). Kwamba pamoja na vielelezo vyote vya uharamia wake bado aling’ang’ania yeye ni msafi na akataka kuendelea kuongoza shirikisho hilo.


Kubenea ana roho ngumu kama Michel Platini, yule alikuwa Rais wa Umoja wa Vyama vya Soka Ulaya (Uefa). Kwamba pamoja na kila ushahidi kudhihirisha umafia wake wa kimtandao kwenye soka, bado alisimama imara kudai anaonewa.


Mwisho kabisa, Blatter na Platini, wamefungiwa na Kamati ya Maadili ya Fifa, kujihusisha na shughuli zote za soka kwa kipindi cha miaka nane.


Kubenea ni mwanaproganda asiyeuonea aibu uongo wake. Ni kama Muhammad Saeed al-Sahhaf, yule aliyekuwa waziri habari wa Iraq, wakati wa utawala wa hayati Saddam Hussein. Al-Sahhaf ndiye aliweka rekodi ya kuwa msema uongo bora mwaka 2003.


Wakati Marekani ilipoivamia Iraq mwaka 2003, Al-Sahhaf alikuwa na kazi ya kusema tu uongo kuwatisha Wamarekani. Tangu walipoanza mpaka walipouteka mji wa Baghdad, hakuna popote ambapo maneno ya Al-Sahhaf yalikuwa kweli.


Kubenea yupo vitani na Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe. Anamshambulia mfululizo. Amejaliwa kumiliki magazeti, basi kwa vile mwenzake hana, ndiyo kila siku anaye tu!


Unaweza kutafuta mahali ambako Zitto na Kubenea waliwahi kugombana, huwezi kupaona. Zaidi, zipo taarifa kuwa Zitto amewahi kuwa msaada kwa Kubenea katika kazi zake.


Kwa nini kila siku Kubenea juu ya Zitto? Huwa anamtafuta nini? Kama kungekuwa na utofauti wa kijinsia kati yao, pengine ipo hoja ingezungumzwa. Ila kwa nidhamu kabisa lipo swali; Ya nini kila siku mwanaume juu ya mwanaume mwenzako? Unamfuatafuata wa nini? Kipi unakitafuta?


Upo msululu wa makala za Kubenea dhidi ya Zitto. Kwa Kubenea, Zitto hajawahi kuwa na jema kwake tangu mwaka 2009. Ni ajabu kuwa katika kipindi chote hicho Zitto hajawahi kujishughulisha kumjibu.


Hiyo inatoa picha moja kubwa kwamba Kubenea ni mwathirika wa maisha ya Zitto. Maana kuchukia kila kitu cha mtu ni ugonjwa. Kwani chochote atakachokifanya kitakupa majeraha.


Hata mwandishi mashuhuri, Marty Rubin aliwahi kusema: “To hate everything is to be wounded by everything.”


Kiswahili: Kuchukia kila kitu ni kujeruhiwa na kila kitu.


Tangu mwaka 2009, vipo vipindi vingi vya ushindi kwa Zitto. Katika maisha yake kisiasa jukwaani, jimboni na bungeni. Fikiria Kubenea ameumia kiasi gani katika kipindi chote hicho ambacho Zitto amekuwa akifanya vizuri.


Katika Uchaguzi Mkuu 2015, Kubenea aliandika makala kuwa Zitto hatashinda ubunge, matokeo yake asiyempenda alishinda. Hayo ni maumivu kiasi gani kwake?


Zitto alishinda na kurejea bungeni mwaka 2010, akashinda uenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (Poac). Kubenea aliandika kuwa Zitto alisaidiwa na Rais wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete. Aliumizwa na ushindi huo!


Mwaka 2012 Zitto alionesha utaalam wake wa siasa za ndani ya bunge, pale wabunge walipopaza sauti kutaka mawaziri nane wang’oke kutokana na ufisadi, vilevile kushindwa kwao kusimamia ofisi walizokabidhiwa.


Zitto akasimama, akasema wabunge wanahangaika kwa sababu hawana mamlaka ya kuwajibisha mawaziri. Ila yupo mmoja ambaye akishughulikiwa, wengine wote watawajibika. Akamtaja huyo kuwa ni waziri mkuu.


Akaanza kukusanya saini za wabunge, kutimiza 70 ili awasilishe hoja ya kumng’oa waziri mkuu. Zitto alifanikiwa kushawishi wabunge wa vyama vyote bungeni ambao walisaini. Saini zikatimia. Rais Kikwete naye akawang’oa mawaziri waliokuwa wanatakiwa kuwajibishwa na kumuokoa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.


Kwa kuchukua mantiki ya maneno ya Rubin, hili nalo lilikuwa shoka la kichwa kwa Kubenea kutoka kwa Zitto. Maana mafanikio ya Zitto ni pigo kwake. Anaumizwa na chuki zake. Chuki zikizidi ni ugonjwa usiotibika.


Mwaka 2012 Poac ilivunjwa na Spika wa Bunge la 10, Anne Makinda. Kubenea akafurahia kwa sababu Zitto alipoteza uenyekiti wa kamati bungeni.


Makinda akaiunganisha Poac na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto akashinda uenyekiti wake, kwa mara nyingine Kubenea alinuna; “kwa nini kila siku Zitto haporomoki?”


Kuelekea mwishoni mwa mwaka 2014, Zitto aliiongoza PAC kwa mafanikio, kuiwajibisha serikali kutokana na wizi mkubwa uliofanyika Benki Kuu kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.


Zilikuwa fedha za mgogoro kati ya Tanesco na mwekezaji, Kampuni ya Independent Power Tanzania Ltd (IPTL). Zikachotwa bila utaratibu. Watu waliiba.

Post a Comment

0 Comments