Kiwanja kilichoshika namba moja kwa kuwa busy kuliko vyote duniani ni kiwanja cha Atlanta Georgia Marekani wanakotoka mastaa kama rapper T.I ambacho kwa mwaka 2013 pekee kimehudumia abiria milioni 94.4, namba mbili inashikwa na Beijing Capital International Airport ambacho kilihudumia abiria milioni 83.7
Kiwanja cha ndege Dubai kimeshika namba 7 kutoka namba 10 mwaka uliopita ambapo kimehudumia abiria milioni 66.4 ambapo kiwanja cha ndege cha Paris kimeshuka nafasi moja kutoka ya 7 mwaka uliopita na kushika ya nane mwaka huu, ya tisa imeshikwa na kiwanja cha ndege cha Dallas/Fort na namba 10 imeshikwa na kiwanja cha Jakarta Indonesia.
credt: millardayo.com
0 Comments